UTU
Utu
wa mtu ni utu, hata kama hana kitu,
Kitu
kwa mtu si kitu, bali utu ndio kitu,
Na
utu ukifurutu, mtu huwa kweli mtu,
Utu
wa mtu ni utu, katu kitu sio utu.
Mtu
aliye na utu, watu humuona mtu,
Hata
kama hana kitu, utu wake huwa kitu,
Kwa
hiyo utu wa mtu, si kitu bali ni utu,
Utu
wa mtu ni utu, katu kitu sio utu.
Kwa
mtu aso na kitu, utu wake ndio kitu,
Utu hubadili
mtu, aso kitu huwa mtu,
Ila
aliye na kitu, hawi mtu bila utu,
Utu
wa mtu ni utu, katu kitu sio utu.
Kwa
mtu alo na kitu, hawi mtu pasi utu,
Utu
wake huwa kutu, hata kama ana kitu,
Kitu
pasipo na utu, ni sawa na ukurutu,
Utu
wa mtu ni utu, katu kitu sio utu.
Kwa
mtu utu ni kitu, hata kama hana kitu,
Utu
ndio kila kitu, kwa mtu kuitwa mtu,
Mambo
aweza kufutu, dalili zikathubutu,
Utu
wa mtu ni utu, katu kitu sio utu.
Utu humfanya
mtu, awe mwenye kuthubutu,
Utu
waondoa kutu, sanjari na utukutu,
Utu wabadili
mtu, aso mtu huwa mtu,
Utu
wa mtu ni utu, katu kitu sio utu.
Tamati
naenzi utu, katu simuenzi mtu,
Mola
tupe watu utu, si tija kutupa kitu,
Utu
ukishafurutu, mtu atapata vitu,
Utu
wa mtu ni utu, katu kitu sio utu.
TAMATI
No comments:
Post a Comment